Pages

E FM

E FM
97.3

Sunday, 27 July 2014

ORODHA KAMILI YA WASHINDI WA TUZO ZA AFRIMMA 2014 DIAMOND NA LADY JAYD WAKIWEMO

Screen Shot 2014-07-27 at 9.43.50 AM
Best DJ Africa 2014- Dj Black (Ghana)
 Best African DJ USA 2014 – Dj Josh (Kenya)
 Best Video of the Year 2014- Flavour (Nigeria)
Best Male East Africa 2014- Diamond (Tanzania)

 Best Male West Africa 2014- Davido (Nigeria)
 Best Female East Africa 2014- Lady Jaydee (Tanzania)
 Best Female West Africa 2014 – Tiwa Savage (Nigeria)
 Best Male Central Africa 2014 – Fally Pupa (Congo)
 Best Female Central Africa 2014- Gasha ( Cameroon)
 Best Male Southern Africa 2014- Khuli Chana (South Africa)
 Best African Group 2014- P-square (Nigeria)
 Best Male Diaspora 2014- Fuse ODG (Ghana)
 Best Female Diaspora 2014- Les Nubians (Cameroon)
 Best Female Southern Africa 2014- Zahara (South Africa)
 Best Dancehall Artist 2014 – Timaya (Nigeria)
 Best Dance in a Video 2014- Iyanya (Lekwa Ukwu) (Nigeria)
 Best Gospel Artiste 2014- Bahati (Kenya)
 Best Traditional Artist 2014- Flavour (Nigeria)
 Best Newcomer 2014- Stanley Enow (Cameroon)
 Best Video Director 2014- Ogopa Dj’s (Kenya)
 Music Producer of the year 2014- Dj Oskido (South Africa)
 Best Dance Group 2014- Imagineto (Nigeria)
 Best Rap Act 2014- Sarkodie (Ghana)
 Best Collaboration 2014- Mafikizolo ft Uhuru (Khona) (South Africa)
 Song of the Year 2014- Kcee (Nigeria)
 Artist of the Year 2014- Davido (Nigeria)
 Leadership in Music Award 2014- 2face Idibia
 Legendary Award 2014- Yvonne Chaka Chaka
 Transformational Leadership Award 2014- Chief Dr. Godswill Akpabio

HONGERA LADY JAYD

Tunapenda kumpa pongezi za

LAANA...!! AUNT EZEKIEL NA KAJALA WANYONYANA DENDA LIVE...NI AIBU TUPU

HUU NDIO MUONEKANO MPYA WA DIAMOND PLATNUMZ...NI MWENDO WA VIPARAAAA...!!

Ni mwendo wa vipaaaaaaaara!!!!!...

Sunday, 20 July 2014

JK AZINDUA RASMI MRADI WA UMEME SONGEA VIJIJINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amezindua mradi wa kusambaza umeme vijijini unaosimamiwa na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) utakaowanufaisha wakazi wa Mkoa wa Ruvuma utakaochangia kuongeza kasi ya maendeleo vijijini.
Rais Jakaya Kikwete yuko katika  ziara yake ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo katika mkoa huo lengo likiwa ni kutimiza azma ya serikali ya kuwa kila mwananchi anapata huduma ya nishati ya umeme. 

 Kwa upande wake Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo amewahakikishia wakazi hao kwamba hadi ifikapo mwezi Novemba mwaka huu vijiji vyote vilivyoko katika mradi wa kusambaza umeme vijijini awamu ya II watakuwa tayari wanatumia nishati hiyo kwa wale watakao wamemudu gharama ya Shilingi Elfu Ishirini na Saba ya kuunganishiwa nishati hiyo.
Imeelezwa kwamba mradi wa usambazaji wa umeme vijijini katika mkoa wa Ruvuma utagharimu kiasi cha Tsh. 26.53 bilioni zitakazohusisha ujenzi wa njia za umeme zenye msongo wa kilovolti 33 zenye jumla ya urefu wa km 538, ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovolti 11 yenye urefu wa km 23, ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa km 272, ufungaji wa transfoma 129 za ukubwa mbalimbali pamoja na kuunganisha wateja 7,488. 

 Mradi huu utatekelezwa na kampuni ya Lanka Transfomers Limited, (LTL) ya nchini SRILANKA kwa mkoa wa Ruvuma. Mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Juni 2015 na kunufaisha wakazi wa wilaya za Songea, Tunduru, Mbinga na Nyasa. 

 Pamoja na uwepo wa mradi huo pia kuna mradi wa kuongeza nguvu ya umeme kwenye wilaya za Mbinga na Tunduru unaotekelezwa na kampuni ya Taikai Co.Ltd ambapo tayari amekamilisha survey ya vituo vyote na ameshawasilisha transifoma ya kituo cha Tunduru. Prof. MUHONGO amesema mradi wa kuongeza nguvu ya umeme utagharimu kiasi cha pesa za kitanzania Shilingi bilioni 2.27 zitakazohusisha ujenzi wa vituo viwili vya kuongeza nguvu ya umeme kutoka kilovoti 11 hadi kufikia kilovoti 33 kwa ajili ya kufikisha umeme katika vijiji vilivyoko mbali. 

Vituo hivyo vitakuwa na transifoma zenye uwezo wa kilowati 3,000 (3.0MW) kila kimoja. Kwa upande wake Mbunge wa MBAMBABAY Captain JOHN KOMBA ameishukuru serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kutekeleza ilani ya uchaguzi ya chama hicho ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara hasa madaraja, kuwawekea umeme, na kupandishwa hadhi kituo cha afya na kuwa hospitali ya wilaya. 

 Miradi ya REA awamu ya II imeanza kutekelezwa rasmi Novemba 2013 na inatakiwa kukamilika ifikapo Juni2015 kwa nchi nzima hivyo kuchangia katika kuongeza kiasi cha wananchi waliofikiwa na huduma ya umeme kufikia asilimia 30.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akielekea eneo la jukwaa mara baada ya kuwasili katika eneo palipofanyika uzinduzi wa mradi wa kusambaza umeme vijijini unaosimamiwa na Wakala wa Umeme Vijijini (REA) wilaya ya Nyasa mwishoni mwa wiki, kushoto kwake ni Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo.
Meneja wa Shirika la umeme nchini, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi,   Bi Salome Nkondola akiwasilisha taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi ya umeme kwa mkoa wa Ruvuma mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya KikweteRais Jakaya M. Kikwete akichukua mkasi kwa ajili ya kukata utepe tayari kuelekea katika eneo la uzinduzi wa mradi wa usambazaji wa umeme wilayani Nyasa mkoa wa Ruvuma, kulia kwake ni Waziri mwenye dhamana na nishati Prof. Sospeter Muhongo.Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete pamoja na viongozi wa serikali wakiwepo Waziri wa Ardhi na maendeleo ya Makazi, Waziri wa Nishati na Madini, Waziri wa Ujenzi wakiwa wameshika utepe tayari kwa Rais kuukata na kuelekea kubonyeza kitufe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mradi huo wa umeme.Rais akifunua kitambaa mahali palipowekwa kitufe kwa ajili ya uzinduzi rasmiRais akifunua kitambaa mahali palipowekwa kitufe kwa ajili ya uzinduzi rasmiRais akibonyeza kitufeRais akifurahia uzinduzi mara baada ya zoezi hilo kukamilika
Burudani wakati wa sherehe hizo
Jiunge na mi kwa kubonyeza kwenye link zifuatazo chini ili kupata habari mpya zaidi. 

          FACEBOOK >>> TWITTER  >>> MATUKIO KWA NJIA YA SAUTI